MAELEKEZO MUHIMU1.
Hakikisha kuwa unayo Ratiba ya Mtihani ya mwaka 2026 iliyoandaliwa na Baraza la Mitihani la Tanzania
2.Hakikisha kwamba unasoma jina la somo juu ya bahasha husika na kuthibitisha kuwa somo hilo ndilo linalostahili kufanyika wakati huo kulingana na Ratiba ya Mtihani.
3.Kabla ya kufungua bahasha, mpe Mtahiniwa asome kwa sauti jina la somo lililoandikwa juu ya
bahasha ili kuthibitisha ni somo husika kwa mujibu wa ratiba.
4.Endapo utata utajitokeza kati ya maelekezo yaliyomo katika Karatasi ya Mtihani na Ratiba ya Mtihani, maelekezo yaliyomo katika karatasi ya Mtihani husika ndiyo yatakayofuatwa.
5.Watahiniwa wenye mahitaji Maalum (Wasioona, Uoni hafifu, Viziwi) waongezewe MUDA WA ZIADA WA DAKIKA 20 KWA KILA SAA kwa somo la Hisabati na DAKIKA 10 KWA KILA SAA kwa masomo mengine.
6.Watahiniwa wenye UONI HAFIFU wapewe karatasi za Mtihani zenye maandishi yaliyokuzwa, zilizoandaliwa na Baraza la Mitihani la Tanzania kwa matumizi yao.
7.Watahiniwa waelekezwe; (a) Kuingia ndani ya chumba cha Mtihani nusu saa kabla ya muda wa Mtihani na watakaochelewa kwa zaidi ya nusu saa baada ya Mtihani kuanza hawataruhusiwa.
(b) Kufuata maelekezo yote yatakayotolewa na wasimamizi wa Mtihani.
(c)Kuandika namba ya Mtihani kwa usahihi.
(d)Kutofanya mawasiliano ya maneno au kwa njia yoyote baina yao. Ikiwa Mtahiniwa ana
tatizo anatakiwa kunyoosha mkono ili kuomba msaada kwa msimamizi wa Mtihani.
(e)Kutojihusisha na vitendo vya udanganyifu katika Mtihani kwani watakaojihusisha
