Ransomware attacks ni nini? Na inafanya shughuli gani

> "© 404 Rights Not Found – Green hacker didn’t ask for them anyway

Ransomware Attacks🧄 (Mashambulizi ya Ransomware)* ni aina ya uhalifu wa kidijitali ambapo hacker hutuma programu hatari (malware) inayofunga au kuficha mafaili kwenye simu au kompyuta yako. Ili uyafungue tena, unalazimika *kulipa fedha (mara nyingi kwa njia ya crypto)

😎
Mfano halisi
:

- 🧄Hacker anaweza kukutumia link kwa email au WhatsApp. Ukifungua tu, ransomware inajipachika na kufunga data zako.

- 🧄Utaona ujumbe ukisema: “Data zako zimefungwa. Lipa BTC 300 ili uzifungue.”

Hatari zake:

- 🧄Biashara zinaweza kusimama.

🧄 Watu hupoteza picha, nyaraka, au kumbukumbu muhimu.

🧄Wengi hulazimika kulipa bila uhakika wa kurudishiwa data.

🧄Mifano ya kweli usije ukasema greenhacker kajuaje haya note im next level napoteza muda mwingi kusoma mambo ya technology

- 🧄WannaCry attack (2017): Ilidukua kompyuta zaidi ya 200,000 duniani kote, ikiwemo hospitali za Uingereza.

🧄Ni muhimu kufundisha watu kuhusu ransomware kwa sababu inalenga kila mtu – si tu mashirika. pia zipo mtu wangu wa IT TEACH BROSS GROUP namna ya kujikinga pia

Njia kuu za kujikinga na *ransomware attacks* ni hizi:

1. Backup ya data mara kwa mara

- 🧄Hifadhi mafaili yako muhimu kwenye external drive au cloud. - 🧄Ukidukuliwa, unaweza kurejesha data bila kulipa.

2. Usifungue link au attachment zisizojulikana

-🧄 Kama email au meseji ina link ya ajabu, hata kama ni kwa jina la rafiki, *usibonyeze*.

3. 🧄Tumia antivirus bora na updated - Antivirus husaidia kugundua na kuzuia ransomware kabla haijafanya madhara.

4. 🧄Update software zako zote - Hacker hutumia mapungufu ya zamani kwenye apps au OS. Update hufunga mapungufu hayo.

5. Epuka kutumia software zilizopigwa crack

- 🧄Mara nyingi zina malware ndani yake. Tumia programu halali tu.

6. 🧄Tumia firewall na VPN unapokuwa online

- 🧄Hii hupunguza uwezekano wa kufuatiliwa au kushambuliwa moja kwa moja.

7. Elimu kwa wengine -🧄 Fundisha marafiki, familia au wanafunzi kuhusu hatari ya ransomware – elimu ni kinga bora.

Zingatia haya ya ziada ili kuimarisha ulinzi dhidi ya ransomware: 8. 🧄Tumia two-factor authentication (2FA)

-🧄 Hata kama hacker ana password yako, hatoweza kuingia bila uthibitisho wa pili. 9.🧄 Dhibiti ruhusa za apps

- 🧄Usiruhusu apps zisizo muhimu kufikia mafaili au mfumo mzima wa simu/kompyuta yako.

10. 🧄Tambua dalili za ransomware mapema

-🧄 Kompyuta kuwa slow, mafaili kubadilika majina au kuwa na extension ngeni (kama .locked) ni ishara.

11. 🧄Usilipe ransom

- 🧄Hakuna uhakika kuwa utarudishiwa data zako. Kulipa kunawapa nguvu hackers. 12. 🧄Tumia strong passwords tofauti kwa kila akaunti

- Epuka kutumia password moja sehemu nyingi. Tumia password manager kama LastPass au Bitwarden.

13. *Jifunze kwa matukio ya wengine*

- Soma visa vya mashambulizi yaliyotokea ili ujifunze mbinu za kujikinga. > "© 404 Rights Not Found – Green hacker didn’t ask for them anyway
Mpya zaidi Nzee zaidi

ads

Magspot Blogger Template
Magspot Blogger Template

نموذج الاتصال